BASI LANGONGANA USO KWA USO NA BAJAJI, MMOJA AFARIKI 7 WAJERUHIWA
Mtu mmoja amefariki na wengine saba kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari la abiria aina ya Tata yenye namba za usajili T 596 EAF inayofanya safari zake Morogoro _Mlimba kugongana uso Kwa uso na bajaji iliyokuwa inatokea Mindu kuelekea Morogoro Mjini.
Mmoja wa Majeruhi hao amesema ajali hiyo imetokea katika eneo la Mindu Barabara kuu ya Morogoro _Iringa majira ya asubuhi moja asubuhi huku chanzo chake kikiwa ni uzembe wa dereva wa basi la abiria kuhama upande wake bila kuchukua tahadhari na kuigonga bajaji hiyo
Post a Comment