Header Ads

test

UBALOZI WA TANZANIA NCHINI PARIS WAONGOZAA USHIRIKI WA WADAU MAONESHO YA UTALII YA B-TRAVEL

 

Na Mwandishi Wetu, Barcelona 


UBALOZI  wa Tanzania nchini Ufaransa ambao unawakilisha pia nchini Uhispania, kwa kushirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), umeratibu na kuongoza ushiriki wa makampuni kadhaa ya utalii kutoka Tanzania katika Maonesho ya Utalii ya B-Travel yaliyoanza Machi 15 Machi, 2024, mjini Barcelona, Falme ya Uhispania.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Ubalozi huo imesema kwamba maonesho hayo ya siku tatu yana lengo la kuwawezesha wenyeji wa Barcelona wenye wa asili ya Catalunya (Catalans) ambao wana desturi ya kutembelea kwa wingi maonesho hayo kutafuta maeneo ya kutembelea wakati wa majira ya kiangazi yanayokaribia kuanza. 

Wakati wa ufunguzi, Waziri wa Biasahara na Kazi Roger Torrent i Ramio alitembelea banda la Tanzania na kushukuru kwa ushiriki wa Tanzania kwa kueleza  Tanzania na Zanzibar ni maeneo yanayovutia watu wengi kuyatembelea kwa sasa na kwamba anategemea mafanikio makubwa ya Tanzania katika sekta ya utalii.

No comments