Header Ads

test

WAUMINI KANISA BAPTIST KINONDONI WAANDAA IBADA MAALUM KULIOMBEA TAIFA

WAUMINI wa Kanisa la Baptist Kinondoni mkoani Dar es Salaam  wakiongozwa na  Mchungaji wa kanisa hilo Samweli Kabonaki wamefanya ibada maalum ya kuliombea Taifa la Tanzania katika kipindi cha majanga yakiwemo mafuriko yanayosababishwa na vua zinazoendelea kunyesha sehemu mbalmbli za nchi yetu na nchi jirani.Akizungumza wakati wa ibada hiyo ,Mchungaji Kabonaki amesema Watanzania na Dunia wanajua kipindi wanachopitia kutokana na uwepo wa majnga yanayoleta madhara katika maeo mbalimbali ya nchini na nje ya nchi."Tumeona  ni vema Kanisa hilo likafanya maombi maalum kuombea nchi yetu na mataifa mengine na duna kiujumla,"amesema na kusisitiza katika kukabiliana na majanga hayo ni vema kila mmoja wetu akamtanguliza Mungu zaidi na yvema ikajulikana Mungu ambaye ndiye mwenye majibu yote na  ni mponyaji Mkuu."




Ibaada ikiendelea

Waimbaji wa kwaya ya Shalom wakiimba wakati wa ibaada ya maalum ya kuliombea Taifa la Tanzania katika kipindi hiki cha majanga mbalimbali leo  Mkoa wa Dar es Salaam.













 

No comments