Header Ads

test

MALORI 120 HUBEBA MAKAA YA MAWE KWA SIKU MGODI WA JITEGEMEE MBINGA

 



Meneja Uchimbaji wa kampuni ya Mgodi wa Makaa ya Mawe ya JITEGEMEE Wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma Bosco Mabena amesema malori zaidi ya 120 hubeba makaa ya mawe kwa siku katika mgodi huo na kwamba uzalishaji wa madini hayo unafanyika kwa njia za kisasa.

Mabena amesema hayo wakati anatoa taarifa ya uchimbaji madini ya makaa ya mawe kwa viongozi kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) ambao wapo mkoani Ruvuma kwenye kampeni ya kuhamasisha uwekezaji wa ndani na usajiri wa biashara TIC.

Amesema makaa ya mawe yanayozalishwa kwenye mgodi wa JITEGEMEE hutumika katika viwanda vilivyopo ndani ya nchi,Afrika Mashariki na nchi za Ulaya na China.

Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa kuzalisha makaa ya mawe nchini ambapo hadi sasa kuna Kampuni za kuchimba makaa ya mawe zaidi ya 22 katika Wilaya za Mbinga ,nyasa na Songea .

Meneja Uzalishaji Madini ya Makaa ya Mawe Mgodi wa JITEGEMEE Mbinga Bosco Mabena akieleza namna Kampuni ya JITEGEMEE inavyozalisha makaa ya mawe
baadhi ya malori yakishusha na kupakia makaa ya mawe katika bandari ya nchi kavu wilayani Mbinga mkoani Ruvuma ambapo kila siku kati ya malori 100 hadi 12o hupakia makaa ya mawe kwenye mgodi hu

No comments